Swahili
Sorah Al-A'la ( The Most High ) - Verses Number 19
سَبِّحِ اسْمَ رَبِّكَ الْأَعْلَى 
( 1 )  
Litakase jina la Mola wako Mlezi aliye juu kabisa,
الَّذِي خَلَقَ فَسَوَّىٰ 
( 2 )  
Aliye umba, na akaweka sawa,
وَالَّذِي قَدَّرَ فَهَدَىٰ 
( 3 )  
Na ambaye amekadiria na akaongoa,
وَالَّذِي أَخْرَجَ الْمَرْعَىٰ 
( 4 )  
Na aliye otesha malisho,
فَجَعَلَهُ غُثَاءً أَحْوَىٰ 
( 5 )  
Kisha akayafanya makavu, meusi.
سَنُقْرِئُكَ فَلَا تَنسَىٰ 
( 6 )  
Tutakusomesha wala hutasahau,
إِلَّا مَا شَاءَ اللَّهُ ۚ إِنَّهُ يَعْلَمُ الْجَهْرَ وَمَا يَخْفَىٰ 
( 7 )  
Ila akipenda Mwenyezi Mungu. Hakika Yeye anayajua yaliyo dhaahiri na yaliyo fichikana.
وَنُيَسِّرُكَ لِلْيُسْرَىٰ 
( 8 )  
Na tutakusahilishia yawe mepesi.
فَذَكِّرْ إِن نَّفَعَتِ الذِّكْرَىٰ 
( 9 )  
Basi kumbusha, kama kukumbusha kunafaa.
سَيَذَّكَّرُ مَن يَخْشَىٰ 
( 10 )  
Atakumbuka mwenye kuogopa.
وَيَتَجَنَّبُهَا الْأَشْقَى 
( 11 )  
Na atajitenga mbali nayo mpotovu,
الَّذِي يَصْلَى النَّارَ الْكُبْرَىٰ 
( 12 )  
Ambaye atauingia Moto mkubwa.
ثُمَّ لَا يَمُوتُ فِيهَا وَلَا يَحْيَىٰ 
( 13 )  
Tena humo hatakufa wala hawi hai.
قَدْ أَفْلَحَ مَن تَزَكَّىٰ 
( 14 )  
Hakika amekwisha fanikiwa aliye jitakasa.
وَذَكَرَ اسْمَ رَبِّهِ فَصَلَّىٰ 
( 15 )  
Na akakumbuka jina la Mola wake Mlezi, na akasali.
بَلْ تُؤْثِرُونَ الْحَيَاةَ الدُّنْيَا 
( 16 )  
Lakini nyinyi mnakhiari maisha ya dunia!
وَالْآخِرَةُ خَيْرٌ وَأَبْقَىٰ 
( 17 )  
Na Akhera ni bora na yenye kudumu zaidi.
إِنَّ هَٰذَا لَفِي الصُّحُفِ الْأُولَىٰ 
( 18 )  
Hakika haya yamo katika Vitabu vya mwanzo,
صُحُفِ إِبْرَاهِيمَ وَمُوسَىٰ 
( 19 )  
Vitabu vya Ibrahimu na Musa.